Tetesi zinasema, Wakala wa mshambuliaji wa Juventus Cristiano Ronaldo’, Jorge Mendes ameipatia Manchester City ofa ya kumsajili nyota huyo wa Portugal mwenye umri wa miaka 36.
Tetesi zinasema, Baada ya kukosa mchezo dhidi ya City, Kane ataichezea Spurs katika Ligi ya Europa dhidi ya klabu ya Porugal Paços de Ferreira Alhamisi.
Arsenal imeanzisha tena mazungumzo na Sheffield United juu ya makubaliano ya mlinda lango, 23, wa England Aaron Ramsdale, baada ya Blades kusemekana kwamba wamepunguza dau lao kutoka £35m hadi £24m.

Paris St-Germain haijaondoa uwezekano wa uhamisho wa dakika za mwisho wa viungo wa kati raia wa Ufaransa Paul Pogba, 28, kutoka Manchester United na Eduardo Camavinga,10 kutoka Rennes.
Tottenham inafikiria uhamisho wa mlinzi wa Chelsea Kurt Zouma. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa, 26, pia amehusishwa na uhamisho wa West Ham msimu huu.
Tetesi zinasema, Atletico Madrid imeiambia Arsenal na Manchester United kwamba beki wa kulia wa England Kieran Trippier, 30, hauzwi.
Tetesi zinasema, Martin Odegaard amekamilisha uhamisho wa kutoka Real Madrid hadi Arsenal mapema leo, baada ya kutoshiriki mazoezi na timu ya Real siku ya Jumanne.
Tetesi zinasema, Wolverhampton Wanderers inajitayarisha kutoa ofa ya £21m kwa Valencia ikimlenga winga wa Ureno Goncalo Guedes, 24.

Tetesi zinasema, Kocha wa Newcastle Steve Bruce anamuwinda kiungo wa kati wa Leicester Hamza Choudhury, 23, kwa mkopo.
Tetesi zinasema, Watford inakaribia kukubali kima cha £7.5m kwa ajili ya mlinzi Mbrazil wa klabu ya Torino Lyanco, 24.
Kiungo wa kati wa Manchester United Andreas Pereira, 25, huenda anakaribia kuondoka Old Trafford huku kukiwa na taarifa kwamba anaelekea Flamengo kufuatia mapendekezo mengi ya mkopo kwa Mbrazil huyo.
Ni muda wa kuwa milionea na kasino za mtandaoni za meridianbet, mchezo wa Sahara Riches unakupa nafasi ya kushinda mkwanja mrefu. Matajiri wa jangwani wanataka wakupe mkwanja leo.



Sania+mapua
Sawa
Sarah
Tetesi safi