Jimmy Greaves mshambuliaji wa Uingereza na timu ya Tottenham ambaye alikuwa ni miongoni mwa wachezaji ambao walishinda kombe ka dunia akiwa na timu ya taifa Uingereza afariki dunia akiwa na umri wa miaka 81.
Greaves ambaye anajulikana kama mfungaji aliyekuwa na kipaji cha hali ya juu katika wakati wake, alijenga jina akiwa na chelsea akifunga magoli 132 katika mechi 169, na baadae kwenda kutengeneza ufalme akiwa na Tottenham Hotspur.

Jimmy greaves alizaliwa mwaka 1940 huko East Ham London, na kuanza safari yake ya katika timu ya vijana Chelsea na kuanzia 1957 hadi 1961 na kuamia Ac Milan ambapo alicheza mechi 12 na kufunga magoli 9 tu.
|
MWAKA |
TIMU |
MICHEZO |
MAGOLI |
|
1955 – 1961 |
Chelsea | 157 |
125 |
|
1961 |
Ac Milan | 12 |
9 |
|
1961 – 1970 |
Tottenham | 321 |
220 |
|
1970 – 1971 |
West Ham United | 38 |
13 |
|
1975 – 1976 |
Brentwood |
||
|
1976 -1977 |
Chelmsford |
||
|
1977 – 1979 |
Barnet | 51 |
16 |
| 1979 – 1980 | Woodford |
Pia aliweza kuichezea timu ya vijana Uingereza wenye umri wa miaka 23 mechi 12 na kufunga magoli 13 kuanzia 1957 hadi 1962, na aliitumikia timu ya taifa ya Uingereza kuanzia mwaka 1959 hadi 1967 huku akionekana mara 57 na kufunga magoli 44.
Jimmy Greaves pia alikuwa mchezaji muhimu kwenye mashindano ya kombe la dunia lilichezwa mwaka 1966 na Uingereza kuibuka mshindi wa mashindano hayo huku Greaves akimaliza na kusherekea akiwa majeruhi yaliyomfanya akose mechi ya fainali dhidi ya West Germany.
Unaanzaje siku yako na kuimaliza bila kupitia katika kasino bomba za meridianbettz, mchezo mashuhuri wa Disco Funk unaweza kukufanya uwe mshindi leo hii.!


