Bingwa wa US Open 2019, Juan Martin del Potro amekiri kuwa hivi karibuni anaweza kutangaza kustaafu kwenye mchezo wa tenisi huku akiendelea kupambani na matatizo ya majeraha ya goti.

Bingwa huyo wa US Open 2009 hajacheza kwenye mzunguko tangu 2019 na amevumilia majeraha, ingawa anatarajiwa kucheza Buenos Aires Open wiki hii ikifuatiwa na Rio Open.
“Inaweza isiwe hivyo na labda ni zaidi ya kuaga kuliko kurudi,” Del Potro alisema katika mkutano wa waandishi wa habari wenye hisia.
“Hivi karibuni nimekuwa nikijitahidi sana kuendelea kucheza, lakini nimekuwa nikiishi ndoto mbaya kwa goti langu.
“Kwa miaka mingi, nimekuwa nikijaribu matibabu mbadala na madaktari na njia tofauti za kurekebisha, lakini sijaweza kuifanya.
“Lakini sikuwahi kufikiria kustaafu kucheza tenisi bila kuwa na nafasi ya kusema kwaheri uwanjani – na sikuweza kupata mchuano bora zaidi kuliko Buenos Aires Open.” alisema Del Porto.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.


