Majeraha Kumuweka Dias nje ya Uwanja Wiki Sita.

 

Beki wa Manchester City, Ruben Dias, 24 anatarajiwa kuendelea kuwa nje ya uwanja kwa wiki sita zaidi baada ya kupata majeraha ya nyama za paja.

 

Mpaka sasa, Dias amekosa mechi tatu pekee kati ya mechi 28 ambazo klabu ya Manchester City imecheza katika Ligi Kuu ya Uingereza (EPL).

“Ni mchezaji muhimu ambaye tukakosa huduma zake. Upekee wa mchango wake ni miongoni mwa sababu ambazo zimetudumisha kileleni mwa jedwali la EPL kwa kipindi kirefu,” alisema kocha Pep Guardiola.

Dias sasa anatarajiwa kukosa mechi tano zijazo za Manchester City ambazo watacheza dhidi ya Sporting CP (UCL), Crystal Palace, Southampton, Burnley na Liverpool mtawaliwa.

Dias alijiunga na Manchester City akitokea Benfica ya Ureno kwa dau la €68M mnamo Septemba 2020. Tangu wakati huo, amesaidia City kushinda mechi 26 kati ya 57 bila kufungwa na kuwaongoza kunyanyua taji la EPL na Carabao Cup mnamo 2020-21.


VUNA MKWANJA NA SHINDANO LA EVOPLAY SPRING AWEKING

Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000  katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

SOMA ZAIDI HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.