Kocha wa klabu ya Barcelona Xavi Hernandez amesema kuwa hakuna mchezaji aliyekataa kujiunga na klabu hiyo tokea alipochukua mikoba ya kuionoa baada ya kuulizwa kuhusu kikao chake alichofanya na Erling Haaland.
Xavi hakuweza kuthibitisha wala kukataa kuhusu kikao ambacho alifanya na Erling Haaland nchini Ujerumani, huku akijua kuwa Barcelona ni miongoni mwa vilabu vinavyogambania pamoja Real Madrid na Manchester City, Kupata saini ya mshambuliaji.

“Ni uthibitisho au swali? angalia, mara zote ni vizuri kusajiriwa na Barcelona, kwangu, hii ndio klabu bora duniani, na kiukweli, hakuna hata mchezaji moja ambaye amesema hapana kwa barcelona tangu niwe hapa kama kocha.”
Alipoulizwa ni jinsi gani anawashawishi kuwasajiri wachezaji Xavi aliongezea, “unawaelezea jinsi tunavyocheza na tunavyowafundisha, unawaambia kwamba watakugusa mpira mara 40 kwenye mchezo badala 20.
“Najaribu kuwaacha waijua kuhusu klabu ni jinsi gani jiji lilivyo zuri. Naibadilisha hiyo kuwa nafasi ya dhahabu kwa mchezaji yeyote na aina ya uchezaji ambayo itawafanya wawe bora.”
Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000 katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.


