Juventus wanaweza kulazimika kumrejesha Aaron Ramsey ya Turin, kwa kuwa uhamisho wake wa mkopo kwenda Glasgow Rangers haujatatua matatizo ya kiafya yanayoendelea.
Kiungo huyo ni mmoja wa wachezaji wanaolipwa fedha nyingi katika klabu hiyo ya Serie A, kwani alifika kama mchezaji huru kutoka Arsenal na hivyo alipewa kitita kikubwa cha mshahara chenye thamani ya €7.5m kwa kila msimu.
Hata hivyo, Mchezaji huyo wa kimataifa wa Wales amekuwa na wakati mgumu kuingia uwanjani akiwa na jezi ya Bianconeri kutokana na majeraha ya misuli na kushuka kwa kiwango.

Kumuuza ilionekana kuwa ngumu mnamo Januari, kwa hivyo alitumwa kwa mkopo Glasgow Rangers, kwa matumaini kwamba wangefanya uhamisho huo kuwa wa kudumu.
kwa mujibu wa Tuttosport, Giovanni van Bronckhorst anakaribia nia ya kumbakisha Ramsey hadi Juni 30, akirudisha tatizo moja kwa moja kwa Juventus.
Mkataba wake na Juventus utaendelea hadi Juni 2023, kwa hivyo klabu hiyo inaweza kujaribu kupunguza hasara na kufanya mazungumzo ya kusitisha mkataba wake mapema zaidi.
Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000 katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.


