Atletico Madrid walithibitisha uhai uliosalia kwenye La Liga walipoiondoa Manchester United kwenye Ligi ya Mabingwa pale Uwanja wa Old Trafford Jumanne jioni kwa kukamilisha ushindi wa jumla ya mabao 2-1.

Katika dimba la Wanda Metropolitano, Mashetani Welkundu waliweza tu kutoka sare ya 1-1, baada ya kuongozwa kwa bao la Joao Felix, kisha Anthony Elanga kuisawazishia United ndani ya dakika kumi za mwisho.
Jumanne ilikuwa ngumu kwa United. Wakati huu alikuwa ni beki wa pembeni wa Brazil, Renan Lodi aliyewachapa bao muhimu kwa kichwa dakika nne kabla ya kipindi cha mapumziko.
Akizungumza baada ya mechi, katika maoni yaliyobebwa na Marca, rais wa Atletico Madrid Enrique Cerezo aliulizwa na Juanma Castano kama angependa kuwatoa wapinzani wao wakubwa Real Madrid katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa.
“Jamani. Ningependelea kucheza na Real Madrid kwenye fainali. Wacha tuone ikiwa tunaweza kuwa na bahati mara ya tatu. Lakini tukiipata Real Madrid katika robo fainali itabidi tuheshimu matokeo ya droo. Muhimu ni kwamba kuna vilabu vya Uhispania huko.” – Enrique Cerezo
SHAOLIN FORTUNES 100 ONJA LADHA YA USHINDI
Maana ya ushindi mkubwa ipo hapa katika mchezo wa SHAOLIN FORTUNES 100 ndani ya kasino maridhawa za meridianbettz. Kwa dau dogo unashinda zaidi, unaweza kucheza mara nyingi uwezavyo huku ukifurahia ladha ya ushindi.


