Kiungo wa Liverpool Thiago Alcantara amesema anazingatia zaidi kucheza na timu yake ya sasa hasikilizi kuhusu uvumi unao muhusisha kurejea katika klabu yake ya zamani.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Hispania ni zao la akademi ya La Masia na alicheza katika kikosi cha wakubwa pamoja na kocha wa sasa wa The Blaugrana Xavi.
Kujiunga tena na wakatalunya ndiyo taarifa zinazogonga vichwa vya habari na Thiago bado hajaleta matarajio ambayo wengi walikuwa nayo katika ligi ya Uingereza lakini ametupilia mbali uvumi wa kwamba anaweza kuondoka Anfield katika dirisha la Januari.
Aliulizwa kuhusu tetesi za kurejea Barcelona Thiago aliwajibu maripota: “Ninacheza mpira, si sijihusishi na tetesi.”
“Ninatazamia zaidi majukumu yangu na timu, nina mkataba na nina safari katika ligi ya Premia nikijaribu kutwaa mataji.
Wiki nyingine ya kushinda mamilioni ukiwa na kasino maridhawa za meridianbettz. Mchezo pendwa wa Fai Cai Shen unakupa thamani ya dau lako, kwa kiasi kidogo cha dau unaweza kushinda mkwanja mrefu.


