Kocha mkuu wa timu ya Arsenal, Mikel Arteta amesema yakuwa hajafurahishwa na matokeo ambayo wameyapata usiku wa kuamkia leo kwenye wa nusu fainali ya pili ya Ligi la Europa baada ya kulazimisha sare na Villarreal.
Baada ya ubao wa uwanja wa Emirates kusoma 0-0 katika nusu fainaili hizo imewafanya Arsenal kuishia katika hatua ya nusu fainali kombe hilo, kwa sababu mchezo wao wa kwanza wa Villarreal ilishinda 2-1 dhidi ya Arsenal.
Arteta amesema kuwa walipambana kusaka matokeo ila juhudi ziligonga mwamba mchezo huo jambo ambalo limewafanya washindwe kutimiza malengo yao.
“Tulikuwa tunahitaji kufanya jambo kwa ajili ya mchezo wetu ili kufika hatua ya fainali ila imeshindikana, wachezaji walikuwa chini, ilikuwa kazi kubwa kwangu.
“Bahati mbaya tumeshindwa, tulikuwa na nafasi za kushinda, kuna nafasi mbili ambazo tumetengeneza ila hatukuweza kufunga, basi hamna namna kwa kuwa hatujapata mabao,” amesema Arteta.
TENGENEZA FAIDA KUPITIA MCHEZO WA TITAN DICE UKIWA NA MERIDIANBET KASINO
Unapokuwa kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, huna sababu ya kucheza kwa mashaka. Titan Dice, ni mchezo unaweza kukupatia mamilioni kwa mzunguko mmoja!
Arteta usihuzunike sana..mpira mabadiliko
Asante kwa taarifa
Wala usihuzunike jipangeni upya
Arteta akubali tu matokeo
Arteta kubali tu matokeo mpira dakika 90 uwanjani
Waongeze juhudi
Akubaliane na matokeo
Waongeze juudi
Pole yao