Vilabu vya Tottenham, Arsenal na Bayern Munich vimeingia kwenye mbio za kuinasa saini ya kinda wa Uingereza Djed Spence anayemilikiwa na klabu ya Middlesbrough.

Middlesbrough walimtoa kwa mkopo katika klabu ya Nottingham Forest msimu uliyopita na kinda huyo wa miaka 21 amekua akihitajika na vilaabu kadhaa vya Bundesliga.
Lakini chipukizi huyo wa zamani wa Fulham alikuwa mmoja wa wachezaji bora wa Forest na alichukua jukumu muhimu katika ushindi wa kushangaza wa Nottingham dhidi ya Arsenal na Leicester kwenye Kombe la FA.
Kiwango chake bora kimevivutia vilabu vingi vya Ulaya lakini Bayern kuingia kwenye kinyang’anyiro kinaleta habari mbaya kwa vilabu viwili vya London Kaskazini.
Mkataba wa Spence huko Riverside unaisha 2024 na Boro hawatarajii kuwa naye tena lakini wanaweza kupata pesa ndefu kutoka Spence.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.


