Koeman: Barca Itapata Shida Kama Nitaondoka

Ronald Koeman amezungumzia uvumi unaoendelea juu ya msimamo wake huko Camp Nou, akisisitiza Barcelona “watapata shida” ikiwa hana hatma klabuni.

Koeman alipewa kandarasi ya miaka miwili na Barca wakati alipochukua nafasi ya Quique Setien katika kiti cha ukufunzi mwezi Agosti mwaka jana, lakini sasa anajikuta akipata presha wakati wa kampeni za 2020-21.

Imependekezwa kuwa Mholanzi huyo angeweza kupoteza kazi yake wakati rais ajaye wa klabu atachaguliwa baadaye mwezi huu, na sasa amekiri kutokuwa na uhakika kuhusiana na ikiwa atapewa nafasi ya kubaki kuwa kiongozi hadi 2022.

“Sijazungumza na mtu yeyote. Tunapaswa kusubiri ni nani atakayekuja kama rais na mpango wake,” Koeman aliambia mkutano na waandishi wa habari Jumanne.

“Ikiwa sioni wakati muhimu kwangu tutakuwa na shida, kwa sababu nina mwaka mmoja zaidi kwenye mkataba wangu.”

Kwa sasa Koeman anaiandaa timu yake kwa pambano la nusu fainali ya pili ya Copa del Rey dhidi ya Sevilla, ambapo watakuwa wakijaribu kupindua jumla ya bao 2-0.

Barca pia wako kwenye hatihati ya kutoka Champions League baada ya kupoteza mchezo wa kwanza wa mechi yao ya 16 ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Paris Saint-Germain 4-1, lakini fomu yao ya La Liga imeboreshwa na kusogea mpaka nafasi ya pili.


Ni Muda wa Kuvuna Mkwanja na Jungle Jim and the Lost Sphinx

Hauihitaji kufikira mara mbili ni mchezo gani utakupatia mkwanja ndani ya kasino za Meridianbet. Jiunge sasa ufurahie Jungle Jim and the Lost Sphinx.

  CHEZA HAPA

10 Komentara

    Koeman anawatishia tu wangapi wameondoka

    Jibu

    Koeman Wana mtishia wangapi wameondoka

    Jibu

    Kwa sasa Koeman anaiandaa timu yake kwa pambano la nusu fainali ya pili ya Copa del Rey dhidi ya Sevilla, ambapo watakuwa wakijaribu kupindua jumla ya bao 2-0.

    Jibu

    Taasisi inatakiwa kuendelea kusitawi bila kutegemea mtu. Nadhani haya ni maini yake sidhani kama Barcelona itafungwa na hayo.

    Jibu

    Aende tu Barcelona wako vizuri

    Jibu

    Safari njema uko uendako

    Jibu

    Sio kweli

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Hakuna ukweli hapo

    Jibu

    Mmh aendee tu hivo ni vitisho vya kawaida

    Jibu

Acha ujumbe