Ronald Koeman amezungumzia uvumi unaoendelea juu ya msimamo wake huko Camp Nou, akisisitiza Barcelona “watapata shida” ikiwa hana hatma klabuni.
Koeman alipewa kandarasi ya miaka miwili na Barca wakati alipochukua nafasi ya Quique Setien katika kiti cha ukufunzi mwezi Agosti mwaka jana, lakini sasa anajikuta akipata presha wakati wa kampeni za 2020-21.
Imependekezwa kuwa Mholanzi huyo angeweza kupoteza kazi yake wakati rais ajaye wa klabu atachaguliwa baadaye mwezi huu, na sasa amekiri kutokuwa na uhakika kuhusiana na ikiwa atapewa nafasi ya kubaki kuwa kiongozi hadi 2022.
“Sijazungumza na mtu yeyote. Tunapaswa kusubiri ni nani atakayekuja kama rais na mpango wake,” Koeman aliambia mkutano na waandishi wa habari Jumanne.
“Ikiwa sioni wakati muhimu kwangu tutakuwa na shida, kwa sababu nina mwaka mmoja zaidi kwenye mkataba wangu.”
Kwa sasa Koeman anaiandaa timu yake kwa pambano la nusu fainali ya pili ya Copa del Rey dhidi ya Sevilla, ambapo watakuwa wakijaribu kupindua jumla ya bao 2-0.
Barca pia wako kwenye hatihati ya kutoka Champions League baada ya kupoteza mchezo wa kwanza wa mechi yao ya 16 ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Paris Saint-Germain 4-1, lakini fomu yao ya La Liga imeboreshwa na kusogea mpaka nafasi ya pili.
Ni Muda wa Kuvuna Mkwanja na Jungle Jim and the Lost Sphinx
Hauihitaji kufikira mara mbili ni mchezo gani utakupatia mkwanja ndani ya kasino za Meridianbet. Jiunge sasa ufurahie Jungle Jim and the Lost Sphinx.
warda
Koeman anawatishia tu wangapi wameondoka
Lydia Emmanuel Magoti
Koeman Wana mtishia wangapi wameondoka
David Pere
Kwa sasa Koeman anaiandaa timu yake kwa pambano la nusu fainali ya pili ya Copa del Rey dhidi ya Sevilla, ambapo watakuwa wakijaribu kupindua jumla ya bao 2-0.
Sadick
Taasisi inatakiwa kuendelea kusitawi bila kutegemea mtu. Nadhani haya ni maini yake sidhani kama Barcelona itafungwa na hayo.
Adelta
Aende tu Barcelona wako vizuri
Venerose
Safari njema uko uendako
Hopemwaikuka
Sio kweli
Caroline
Asante kwa taarifa
Angelina
Hakuna ukweli hapo
Neema juma
Mmh aendee tu hivo ni vitisho vya kawaida