Manchester City wapo kwenye mazungumzo ya kutaka kumsajili beki wa kati wa Borussia Dortmund Manuel Akanji.
Mchezaji wa kimataifa wa Uswizi, Akanji yuko katika mwaka wa mwisho wa kandarasi yake na bado hajaonekana katika klabu ya Dortmund msimu huu.
Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola hajakataa kusajili wachezaji wengine kabla ya tarehe ya mwisho ya usajili amabapo alipozungumza na waandishi wa habari katika mkutano wake kuelekea mchezo wa Jumatano dhidi ya Nottingham Forest.
Alipoulizwa kuhusu taarida za usajili, alisema: “Sijui, sijui kitakachotokea.”
Mchezaji huyo amekuwa akilengwa na Inter Milan msimu huu wa joto, kwa mujibu wa SkySport huko Italia.
Taarifa nyingi zimekuwa zikiripoti kwamba Dortmund wanataka kati ya Paundi 13M (€15m) na £17M (€20m) ili kumuuza.