Steve Nicol: Ronaldo Simuelewi.

Gwiji wa Liverpool Steve Nicol alimlaumu Cristiano Ronaldo kwa kushindwa kwa Manchester United na Real Sociedad, kwenye Ligi ya Europa Alhamisi jioni na anaamini kuwa fowadi huyo wa zamani anaonyesha umri wake.

Steve Nicol: Ronaldo Simuelewi.

Ronaldo katika mechi yake ya pili msimu huu, alipata nafasi nyingi dhidi ya kikosi hicho cha Basque lakini alishindwa kubadilisha hata moja kati ya hizo wakati Red Devils walipoteza 1-0, kwa penalti ya kipindi cha pili kutoka kwa Brais Mendez.

Nicol alisema Ronaldo anaonekana ‘kila mmoja kati ya miaka hiyo 37’ alipokuwa akicheza mechi yake ya kwanza ya Ligi ya Europa ndani ya miaka 20 na kusisitiza kwamba kuna ‘kitu kinakosekana’ kutokana na uchezaji wake.

Steve Nicol: Ronaldo Simuelewi.

Kwa jumla, mshindi huyo mara tano wa tuzo ya Ballon d’Or alishindwa kubadilisha nafasi sita kubwa za mabao.

Aliuweka mpira wavuni katika dakika ya 35 baada ya krosi nzuri ya Diogo Dalot, lakini bao hilo likakataliwa baada ya nahodha wa Ureno kuotea.

Akizungumza na ESPN kuhusu uchezaji wake, Nicol alisema: ‘Nitasema ukweli, unapotaja mchezo, kitu pekee nilichonacho kichwani mwangu ni Ronaldo kusafisha [langoni] na kunaswa na wachezaji wawili.
“Hiyo ni aina ya mawazo yangu. Na alikuwa na sura nyingine. Alikuwa na nafasi zingine kadhaa, sio nzuri kama hiyo, lakini kulikuwa na kitu kilikosekana”.

“Hicho ndicho ninachofikiria ninapofikiria mchezo huu. Hakukuwa na mengi ndani yake kati ya pande hizo mbili, sio nafasi nyingi kwenye mchezo, Lakini hilo ndilo jambo pekee ninaloweza kufikiria”. Alisema Nicol

Steve Nicol: Ronaldo Simuelewi.

Kwa mara ya kwanza Ronaldo anacheza mashindano ya Europa tangu kuanza kucheza michezo mbalimbali.

Acha ujumbe