Mechi ya Arsenal ya Ligi ya Europa dhidi ya PSV Eindhoven iliyopangwa kufanyika siku ya Alhamisi tarehe 15 Septemba, 2022 imeahirishwa kutokana na sababu za kiusalama kufuatia kifo cha Malkia Elizabeth II.

Ratiba ya wiki iliyopita ya Ligi Kuu ya Uingereza ilisitishwa kabisa kama ishara ya heshima kufuatia kufariki kwa, Malkia Elizabeth II Alhamisi Septemba 8. Hatua hiyo ilikuwa ya utata baada ya michezo mingine kama kriketi na raga kuamua kuendelea kucheza.
Sasa mchezo mwingine umeahirishwa, huku Arsenal wakIthibitisha kwamba mchezo wao na PSV siku ya Alhamisi kwenye Uwanja wa Emirates umesitishwa baada ya timu hiyo ya Ligi ya Eredivisie kusema UEFA imefikia uamuzi kuhusu mechi hiyo.

“Mchezo wetu wa nyumbani wa UEFA Europa League dhidi ya PSV Eindhoven, uliopangwa kufanyika Alhamisi Septemba 15, umeahirishwa,” taarifa kwenye Instagram ya Arsenal ilisomeka.
“Kuahirishwa huko kunafuatia uhusiano kati ya UEFA, Polisi wa Metropolitan na sisi wenyewe, baada ya kufariki kwa Malkia Elizabeth II.”

Tunashirikiana na mamlaka kupanga tarehe nyingine ya mechi na tiketi zozote (ikiwa ni pamoja na zile zilizonunuliwa kupitia Soko la Tiketi au zilizopokelewa kupitia Uhamisho wa Tiketi) na/au vifurushi vingine vilivyonunuliwa kwa muundo huu vitatumika kwa tarehe iliyoratibiwa upya.

