Mwenyekiti wa Bodi ya Simba SC, Crescentus Magori, ampongeza kikosi chake kwa ubora wa michezo yao na kuhimiza ligi ya Tanzania kuendelea kuwa na ushindani wa kweli.
Akizungumza baada ya mchezo wa ligi dhidi ya Pamba Jiji, Magori alisema.“Ligi nzuri ni ile ambayo kuna timu zake zinafungwa, kusare na kushinda na tukiacha mpira uchezwe bila maigizo ndio tutapata ubora wa ligi yetu, ndio maana mechi zetu zote za Simba SC ni bora hakuna maigizo, mechi za Simba SC ndio zinavutia.”
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Aliongeza kuwa: “Pamba Jiji walikuwa vizuri, walikuwa bora na tunategemea mechi zote acheze hivi ndio tutaona ubora wa ligi yetu, kuna timu hapa utashangaa zinafungwa goli nne hadi tano.”
Kauli hizi zinaonyesha wazi msimamo wa bodi ya Simba SC kuhakikisha kila mechi inakuwa na ushindani wa hali ya juu, huku ikionyesha kuwa mashabiki wanastahili kuona michezo yenye mvuto na ushindani wa kweli.
Magori ameendelea kusisitiza umuhimu wa timu zote kucheza kwa uwazi na bila maigizo ili kuongeza umaarufu na kiwango cha ligi ya Tanzania, ikiwemo kuimarisha michuano ya ligi kuu ya NBC.
Kauli yake pia ni ishara kwa timu nyingine nchini kuwa ushindani wa kweli ndio unachochea maendeleo ya soka na kuvutia mashabiki wengi zaidi kwenye viwanja.

