EPL: Vilabu vyote 20 vya Ligi Kuu ya Uingereza vimeripotiwa kuunga mkono kwa kauli moja mapendekezo ya kulegeza vikwazo juu ya uwezo wao wa kusajili wachezaji kutoka nje ya nchi, na wanaamini FA inachangamsha wazo hilo.
Kwa mujibu wa The Athletic, suala la kulegeza sheria za kusajili wachezaji wa kigeni liliibuliwa katika mkutano wa hivi karibuni wa wawakilishi kutoka kila klabu za Ligi Kuu.
Ripoti hiyo inaendelea kudai kuwa mtendaji mkuu wa FA Mark Bullingham pia alihudhuria mkutano huo mnamo Septemba 21, na kuashiria kuwa na msimamo uliobadilishwa dhidi ya upinzani wa muda mrefu wa Chama cha Soka wa kulegeza vikwazo vilivyowekwa.
Sheria za sasa za vilabu vya Epl kusajili wachezaji kutoka nje ya nchi ziliwekwa Januari 2021 kufuatia Uingereza kujiondoa kutoka Umoja wa Ulaya, ambao ulishuhudia mfumo wa Uidhinishaji wa Bodi ya Utawala (GBE) ulianzishwa na FA.
Hili liliathiri pakubwa wachezaji ambao timu za Epl zinaweza kusajili kutoka nje ya Uingereza, huku vilabu vikiwa havina uwezo tena wa kuajiri wanasoka wa kigeni walio na umri wa chini ya miaka 18 huku vilabu vya Uingereza vilihitaji kukidhi vigezo vya GBE kabla ya kupewa kibali cha kukamilisha uhamisho.
Ulikuwa unawaza ni wapi utacheza kasino?, Swali lako limepata majibu Meridianbet Wamekusogezea Mashine za Slot karibu yako Zinapatikana kwenye Maduka yote ya Meridianbet mtaani kwako. Cheza kasino za Slot na Ushinde Bonasi kubwa zaidi.