Mbappe: Ashindwa Kueleza Nani Bora Kati ya Messi & Ronaldo

Kylian Mbappe ameshindwa kuchagua ni mchezaji gani kati ya Messi na Ronaldo anahisi ni bora zaidi ya mwenzake.

Fowadi huyo wa Ufaransa alikua akimwabudu Ronaldo, lakini sasa anashirikiana na Messi katika klabu ya PSG, hivyo usimfanye achague kati ya hao wawili.

Mbappe: Ashindwa Kueleza Nani Bora Kati ya Messi & Ronaldo

“Nampendelea nani? Ni sawa na kuchagua kati ya baba yako au mama yako, huwezi,” Mbappe alisema.

“Kwa wale wote wa kizazi changu, Ballon d’Or bila shaka inahusishwa na vita kati ya Messi na Cristiano. Nikichimba sana kwenye kumbukumbu yangu, pia namkumbuka kidogo Ronaldinho (mshindi wa Ballon d’Or mwaka 2005).

Mbappe: Ashindwa Kueleza Nani Bora Kati ya Messi & Ronaldo

“Lakini, kusema ukweli, kila kitu kimekandamizwa na wale wawili wenye tamaa! Wameshiriki tuzo kwa muda mrefu sana. Kila mwaka, kama kila mtu mwingine, nilijiuliza ni yupi kati yao angepata. Nikiangalia nyuma, vita hivyo vilikuwa hatari sana.”

Tuzo kumi na mbili za Ballon d’Or, takriban mabao 1500 ya klabu na msururu kamili wa vikombe kati yao. Kuchagua kati ya Messi na Ronaldo si kazi rahisi.

Mbappe: Ashindwa Kueleza Nani Bora Kati ya Messi & Ronaldo

Bado, umeona maoni ya baadhi ya wachezaji bora duniani wa zamani na wa sasa, kwa hiyo wewe unamchagua nani?

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.