Roma wakamilisha Usajiri wa Paulo Dybala

Mshambuliaji wa kimataifa kutoka nchini Argentina Amejiunga rasmi na klabu ya Roma kwa uhamisho huru na kusaini kandarasi ya miaka mitatu huku kukiwa na kipengere cha thamani ya €20milion kwa klabu itakayotaka kuvunja mkataba wake.

Paulo Dybala kabla ya kusaini Roma alihusishwa na vilabu vingi barani Ulaya vikiwemo vilabu vikubwa nchini Uingereza kama Tottenham na Arsenal, Lakini ameamua kubaki nchini Italia.

“Siku ambayo imenipelekea kusaini mkataba huu imejawa na hisia nyingi, uharaka na nia ambayo klabu ya Roma imetumia jinsi ilivyonihitaji mimi imeweka utofauti mkubwa.

“Najiunga kwenye timu ambayo iko kwenye kilele, klabu ambayo imeendelea kuweka misingi imara kwa ajiri mafanikio ya mbeleni, na kufanya kazi na jose mourinho itakuwa ni heshima.”

Dybala kwenye misimu yake saba aliyokuwepo kwenye klabu ya Juventus amefanikiwa kufunga magoli 115 kwenye michezo 293.

 

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.