Ten Hag:Ronaldo Atafunga Sana Utd.

Kocha wa Manchester United Erik ten Hag anatarajia kwamba Cristiano Ronaldo atafunga mabao zaidi akiwa fiti kabisa.

Nyota huyo wa Ureno alifungua akaunti yake ya magoli kwa msimu wa 2022/23 baada ya kufunga kwa penalti katika ushindi wa 2-0 wa Manchester United dhidi ya Sheriff kwenye Ligi ya Europa Alhamisi usiku.

Ten Hag:Ronaldo Atafunga Sana Utd.

Ilikuwa ni mara ya tatu tu ya Ronaldo kuanza kampeni baada ya kujaribu kulazimisha kuondoka Old Trafford wakati wa usajili wa majira ya kiangazi.

Ronaldo alikosa mechi za pre-season kwa sababu binafsi na kumekuwa na maswali kuhusu nafasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 katika mipango ya muda mrefu ya Ten Hag.

Ten Hag:Ronaldo Atafunga Sana Utd.

United wamefurahia kufufuka tangu Ronaldo kutolewa kwenye kikosi cha kwanza baada ya kuchapwa mabao 4-0 na Brentford na kushindwa kwa mara ya kwanza tangu mechi hiyo aliporejea kwenye kikosi dhidi ya Real Sociedad.

Hata hivyo, Ten Hag anasisitiza matumizi yake ya Ronaldo yanazingatia utimamu wa mwili na bado anatarajia mfungaji bora huyo kuwa mchezaji muhimu msimu huu.

Ten Hag:Ronaldo Atafunga Sana Utd.

Mholanzi huyo alisema katika mkutano wake na waandishi wa habari baada ya mechi: “Tunaweza kutarajia hili unapokosa maandalizi ya msimu kwa hivyo anatakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuwekeza ili kupata utimamu sahihi kisha atafunga mabao zaidi.

“Unaweza kuona yuko karibu sana akiimarika zaidi atawamaliza. Nadhani amejitolea kabisa kwenye mchezo huu na amejitolea kabisa kwa timu hii, anahusika kabisa.

Acha ujumbe