AHMED ALLY AWATULIZA MASHABIKI SIMBA

MENEJA wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amewataka mashabiki wa klabu hiyo kuwa na utulivu ili kuwapunguzia presha viongozi wa timu hiyo ili wasifanye maamuzi ambayo sio sahihi kwa timu hiyo ambayo yanaweza kupelekea kufanya vibaya.

Ahmed Ally alisema huu ni muda ambao wanatakiwa kuwa pamoja na kuipambania timu yao ili iweze kufikia malengo, lakini kubwa kuwapa moyo viongozi wao kwenye wakati huu mgumu.AHMED ALLY“Tuwamini viongozi wetu, tukikubali kuchanganyikiwa sasa hata mzunguko wa kwanza bado haujaisha tutapotea sana.

“Timu yetu bado inatakiwa kucheza mechi za ligi zilizosalia na kufanya vizuri kwenye mashindano ya kimataifa,” alisema Ahmed Ally.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.