Klabu ya Azam FC baada ya kumaliza ligi kibabe kwa kuitandika Polisi Tanzania mabao 8-0 jana, leo hii wameanza safari ya kuelekea Tanga ambapo itapigwa fainali ya Kombe la FA.

Azam FC waliingia hatua hii ya fainali kwa kuitoa Simba kwa mabao 2-1 na kujikatia tiketi moja kwa moja ya kucheza fainali huku Yanga wao walimtoa Singida Big Stars.
Wanalamba lamba wamemaliza ligi wakiwa nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wakiwa na pointi zao 59 ambapo watashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika msimu ujao.
Wakati mabingwa wa ligi mara ya pili mfululizo Wananchi wao wamemaliza ligi wakiwa na pointi zao 78, na watacheza Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao huku msimu huu wakiweka rekodi ya kufika Fainali Kombe la Shirikisho CAF.

Mara ya mwisho timu hizi kukutana kwenye ligi, vijana wa Chamazi walipoteza mchezo huo. Je fainali ya Jumapili wanaweza kulipa kisasi huku kukiwa na ongezeko la Feisali Salum?

