Mkurugenzi mtendaji mkuu wa klabu ya Simba Barbara Gonzalez amesema wana mpango wa kuingia kibabe katika dirisha dogo la usajili mwezi Januari.
Klabu ya Simba imeanza kwa kusuasua kwenye ligi kuu ya NBC baada ya kushindwa kuonesha ubora mkubwa kama ambavyo ilidhaniwa mwanzo wa msimu. Kutokana na hali hiyo imewafanya viongozi wa klabu hiyo kufikiria kuingia sokoni kukiboresha kikosi hicho.
Akizungumza na wanahabari Barbara “Tumetenga bajeti ya kutosha ili kuwapata wachezaji wenye ubora kila eneo ambalo limekua na mapungufu kwenye kikosi chetu haswa kwenye mzunguko huu wa kwanza” Simba inahitaji kuboresha timu yao na kuifanya ya kiushindani zaidi haswa kwenye kipindi hichi ambacho matokeo yamekua ya shida.
Mpaka sasa klabu ya Simba inakamata nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi kuu ya Tanzania NBC wakiwa na alama zao 28 huku wakiwa wamewazidi vinara kwa mechi wenye alama 29. Huku kimahesabau Yanga wakishinda michezo yao miwili wanaiacha Simba kwa alama saba.
Klabu ya Simba chini ya Mkurugenzi mkuu mtendaji Barbara wanataka kuhakikisha klabu hiyo inarudi kwa kasi zaidi kwenye mzunguko wa pili na hiyo itakuja baada ya kuingia sokoni na kufanya usajili wa maana.

Je wewe hucheza Kasino Mtandaoni na umekuwa ukijiuliza ni mchezo gani rahisi na mzuri kwa ushindi? Basi Usihangaike Aviator ni rahisi zaidi kucheza na kushinda, kingine cha zaidi ni kwamba Aviator Bonanza imerudi tena Cheza zaidi ujiweke kwenye nafasi ya kushinda Samsung A23.

