BENCHIKHA AWAHOFIA JWANENG GALAXY

Kocha wa Simba Abdelhack Benchikha, amesema kuwa haitakuwa rahisi kucheza na Jwaneng Galaxy kwa kuwa mara zote huwa hawabariki.

“Galaxy sio timu rahisi ni kama jeshi lisilotabirika, hakuna aliyedhani kama ingeifunga Wydad Casablanca nchini Morocco kwenye mchezo wa kwanza wa makundi.benchikha“Hata hapa Simba rekodi zinaonyesha wamewahi kushtua kwa kushinda hapa, nadhani mashabiki na hata wao wachezaji wanalijua hili na tayari nimeshakaa kikao na wachezaji na kuwakumbusha.

Kocha Benchikha alisema“Kwenye soka mambo ya kushtua kama haya huwa yanatokea, sitaki historia hii ijirudie hapa chini yangu, nimezungumza nao tukiwa kule ugenini juzi nadhani kila mtu ataelewa tulizungumza nini.

“Tunatakiwa kujipanga na vita nzito ya mchezo huu, nawaomba mashabiki wetu waje kwa wingi kuwapa hamasa wachezaji wao wakiwa vitani ndio kitu pekee tunahitaji kutoka kwao,”benchikha“Ili kushinda tunahitaji kufunga mabao ya kutosha lakini pia kujilinda vizuri lakini kule mbele bado hatujawa imara zaidi tutawaongezea wachezaji mbinu za kutengeneza nafasi na kuzitumia kwenye hizi siku tutakazokuwa kambini” Alisema Benchikha

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.