Wachezaji wa klabu ya Yanga Bernard Morisson na Stefane Aziz Ki wamerejea ndani ya klabu hiyo baada ya kutokuepo kutokana na changamoto mbalimbali ambazo ziliwakabili.
Mchezaji Bernard Morisson ambaye inasemekana alikwenda nchini kwao Ghana kutokana na matatizo ya kifamilia, Lakini baada ya hapo alionekana akizindua taasisi yake ambayo itakua inashughulika na masuala ya kimichezo na kusaidia vijana nchini kwao Ghana.
Winga huyo machachari ilielezwa inawezekana akapewa adhabu ndani ya timu kutokana na kuchelewa ndani ya timu hiyo, Pia msemaji wa klabu ya Yanga Ali kamwe alieleza suala la mchezaji huyo litatolewa ufafanuzi na klabu hiyo.
Taarifa zilieleza pia kua mchezaji huyo alitakiwa kusimamishwa ndani ya klabu hiyo kutokana na matatizo ya kinidhamu au kuweza kuvunjiwa mkataba, Lakini imebainika kua ni taarifa za uzushi na Bernard Morisson atasalia ku mchezaji wa Yanga na hakuna adhabu itatolewa dhidi yake.
Mchezaji Bernard Morisson na Stefane Aziz Ki wameonekana kwenye kambi ya mazoezi ya mazoezi ya klabu hiyo iliyopo ndani Kigamnboni ikitambulika kama Avic Town. Wachezaji hao wanatarajiwa kuanza kuonekana kwenye michezo ya klabu ya Yanga inayofuata.

