Kikosi cha Pan African, kesho jumatano kinatarajia kuanza mazoezi yake kwa ajili ya kujiweka sawa kuelekea mchezo wao ujao wa ligi dhidi ya Green Warriors.
Mchezo huo wa ligi ya Championship unatarajia kupigwa Januari 14 mwaka huu kwenye Uwanja wa Mej. Isamuhyo, Mbweni Jijini Dar.

Akizungumzia mipango yao, Ofisa Habari wa Pan African, Leen Essau amesema kuwa tayari wameweka mikakati ya kuhakikisha wanarejesha makali yao katika michezo iliyobakia.

“Dirisha la usajili limefunguliwa tayari hivyo kwa sasa tunakamilisha baadhi ya sajili za wachezaji ili ligi itakaporejea tuweze kuwatumia katika kurejesha makali yetu.
“Kikosi kinatarajia kuanza mazoezi kesho jumatano kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wetu dhidi ya Green Warriors utakaopigwa Januari 14 mwaka huu.”

