Kiungo wa Juventus Adrien Rabiot amesema kuwa kocha mkuu wa timu hiyo Massimiliano Allegri ni kocha kamili na ana uwezo wa kubadilisha msimu wa Juventus.

Allegri alishinda mataji 11 katika kipindi chake cha kwanza cha misimu mitano akiwa na Juve, lakini yuko kwenye presha kubwa mwaka mmoja na nusu baada ya kurejea kwenye Uwanja wa Allianz.
Juventus walimaliza katika nafasi ya nne katika Serie A msimu uliopita na walimaliza kampeni bila kombe kwa mara ya kwanza tangu msimu wa 2010-11. Bianconeri wameanza msimu huu taratibu, huku wakipokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa AC Milan Jumamosi.

Rabiot alimuunga mkono Allegri ambae kwasasa anaonekana kukishindwa kikosi hicho, kabla ya mechi ya Ligi ya Mabingwa kati yao dhidi ya Maccabi Haifa siku ya Jumanne, ambapo mchezo wa kwanza Juventus walishinda kwa mabao 3-1. Rabiot alisema;
“Anajua kusimamia timu, ndani na nje ya uwanja. Sio kila mtu anaweza kufanya hivyo. Kwangu mimi, yeye ni kocha kamili, ndani na nje ya uwanja.”


