Ukisikia siku ya kufa nyani miti yote huteleza, ndio maisha ya Antonio Conte na Inter Milan kwenye Ligi ya Mabingwa msimu huu.
Hii ni mara ya kwanza kwa Inter kutopata ushindi kwenye mchezo wowote kwa mechi nne mfululizo kwenye mashindano ya Ulaya.
Antonio Conte ameshuhudia timu yake ikiambulia kipigo kingine kutoka kwa Real Madrid jana usiku. Matokeo ambayo yanaifanya Inter ishike mkia kwenye Kundi B wakiwa pointi 5 nyuma ya Madrid (nafasi ya 2) na pointi 6 nyuma ya vinara wa kundi hilo Borussia Monchengladbach.
Baada ya kipigo hicho (2-0), kocha Antonio Conte atoaneno. Conte ameiambia Sky Sport Italia “siku zote itaendelea kuwa ngumu kucheza na timu kama Real Madrid kwa hiyo unapokuwa umeshafungwa goli moja na unapungufu ya mchezaji mmoja, unakuwa na kazi kubwa ya kuupanda huo mlima.
“Ninadhani tumeona tofauti yao na sisi. Isituvunje moyo, imetuonesha ni njia gani tunapaswa kuifuata.
“Tunatakiwa kuwawatulivu na kuongeza juhudi zaidi, tutambue ni wapi tupo na tusiyumbishwe na maneno ya watu wa nje.
“Njia sahihi zaidi ni kufanya kazi kwa bidii na kukua kwa kila linalowezekana.”
Kupoteza mchezo dhidi ya Madrid kunayaweka matatani matarajio ya Inter kufuzu hatua ya 16 bora. Mpaka sasa Inter wanapointi 2 pekee katika michezo 4 waliyocheza.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.



Tatu
Antoni conte anatakiwa kujipanga upya
Ester jackson
Conte anatakiwa kuwa makini na mbinu zake siku ya Leo asije akapoteza mechi
Khadija
Ajipange upya
Lydia Emmanuel Magoti
Anatakiwa ajipange upya
magdalena
ajipange ili aweze kujua ni wapi amekosea ili atengeneze upya
Dorophina
Inter kwa sasa wanatakiwa kujipanga vizuri
Saupha mohamed
Wajipange sasa
Sarah
Ajipange upya
aisha
Ajipange upya ili asipoteze mechi tena
David Pere
Njia sahihi zaidi ni kufanya kazi kwa bidii na kukua kwa kila linalowezekana.
Genia Sikaluzwe
Wajipange sasa
Hopemwaikuka
Duh
Fatina mfingi
Mmmh
samiah
Duuh
Sauda
Ajipange sana tu
warda
Huwa namwonea sana huruma conte
Farida ahmad
Ajiweke sawa Conte