Kocha mkuu wa klabu ya Arsenal Mikel Arteta amewahimiza wachezaji wake waamini kuwa wanaweza kuendeleza mbio za ushindi kwenye mechi dhidi ya Manchester United licha ya kuwa na matatizo kwenye kikosi.

Aaron Ramsdale pamoja na nahodha Martin Odegaard bado wana shaka ya kutokuwepo lakini kwa upande wa Zinchenko, Thomas Partey, na Mohamed Elneny wakiwa tayari hawapo kwenye kikosi.
Lakini baada ya kupata ushindi kwenye mechi tano mfululizo kwenye ligi hata mara baada ya kushinda mechi yao iliyopita dhidi ya Aston Villa kunawafanya wajiamini kuelekea mchezo huu wa leo ambapo watakuwa ugenini dhidi ya United.

Sare ya Manchester City jana dhidi ya Villa jana inawapa Gunners nafasi ya kusonga mbele kwa alama nne kileleni mara baada ya mechi sita endapo watashinda mechi yao ya leo pale Old Traford. Arteta anasema kuwa,
“Tumeshinda ugenini hapo awali, lazima tufanye hivyo tena na tunaamini tunaweza kwenda huko, kucheza kwa njia yetu na kushinda mechi. Sidhani kama ni suala.


