Berlin Derby Imeisha, Vipi Tena Leo?

Jana kulikuwa na gemu kali sana ya Berlin derby iliyofungua mechiwiki ya 27 ya mashindano ya ligi kuu ya nchini Ujerumani, Bundesliga, ambayo ilirejea tangu wiki iliyopita baada ya kwenda likizo ya lazima.

Hapa ninakuletea mambo muhimu ya kuyatazama sana mwishoni mwa wiki hii katika ligi hiyo. Usisahau kuwa bado unaweza kuzibetia gemu hizo zote hapa hapa na kushinda sana ukiwa nasi.

Ligi hiyo ya Bundesliga inaendelea tena wikiendi hii ikiwa ni muda wa mechiwiki ya 27 kwa sasa na imeanza rasmi jana usiku kukiwa na gemu nzuri sana iliyotoa burudani ya aina yake uwanjani.

Hata hivyo hayo yameshapita, vipi tena leo?

Mbio za top four: Monchengladbach v Leverkusen

Wawili hawa wako katika hali nzuri sana kisoka na wanakutana leo Jumamosi wakiwa wanawania nafasi ya kuingia kwenye nne bora ya ligi yao. Borussia Monchengladbach wanakamatia nafasi ya tatu wakati hawa Bayer Leverkusen wanakalia nafasi ya tano wakiwa na jumla ya alama 50 mpaka sasa, wako alama mbili nyuma ya wapinzani wao wa leo.

Wote hawa wameshinda gemu zao zilizopita lakini hali ya Gladbach awapo nyumbani huwa ni faida kubwa sana kwao. Zaidi ya hayo, Monchengladbach wameshinda mechi zao mbili zilizopita walipokutana pamoja uwanjani. Itashangaza sana kuona kwamba wamewapiga wenyeji wao ambao ni upande wa Peter Bosz wakiwa kwao mara moja pekee katika gemu zao nane zilizopita.

Hatari zaidi pale mkiani

Hawa akina Paderborn na Werder Bremen wapo katika uzi mwembamba sana wa kuharibikiwa mambo yao kwa sasa. Jamaa hawa wawili wanakamatia nafasi mbili za mkiani mwa msimamo wa ligi ya Bundesliga wakiwa na jumla ya mechi nane pekee ili kumaliza msimu huu.

Walio chini zaidi, Paderborn hawajashinda mechi yao yoyote katika gemu zao saba zilizopita kwenye ligi. Wamepoteza mechi tano kati ya hizo. Wakati huo huo, nao Bremen wapo katika msukosuko sana kwa sasa. Mabingwa wa zamani wa Bundesliga wameshinda mechi mbili pekee kati ya sasa na mwezi wa Septemba kwenye ligi yao.

Wamepoteza mechi sita katika mechi zao saba walizocheza. Paderborn anakuwa mwenyeji wa Hoffenheim wakati nao Bremen wanawatembelea wale walio katika nafasi sita za juu, Freiburg. Endapo mfumo wao ukiendelea kuwa sawa na wakati uliopita mambo yanaonekana kuwa mabaya kwa jamaa wote hao.

Bayern na msiba zaidi kwa Frankfurt

Bayern wanarudi uwanjani wakiwa wameshinda mechi yao dhidi ya Union Berlin. Wanatazamia kuimarisha hali yao ya kimchezo wakiwa pale kileleni wakati wanakutana na Frankfurt siku ya leo Jumamosi katika gemu ya jioni kabisa mwa siku.

Monchengladbach v Leverkusen

Hao Frankfurt wapo katika hali mbaya sana kwa sasa. Jitihada zao za kurudi katika mstari zinaonekana kuwa ni majanga zaidi kwao kwani wamekuwa na mafanikio machache sana. Wamepoteza gemu kwa 3-1 walipokutana na Monchengladbach na kuwafanya wawe wamepoteza mechi nne mfululizo katika ligi yao ya Ujerumani.

Wanakalia nafasi ya 13 katika msimamo wa ligi wakiwa na alama tano kuelekea kwenye hatari ya kushuka daraja. Nao Bayern wameshinda mechi zao 11 kati ya mechi 12 walizocheza kwenye ligi, hivyo hawa akina Frankfurt wana kazi nzito na wajipange sana.

31 Komentara

    game ilikuwa kali sana

    Jibu

    Kama naona Dortmund anapoteza leo hivii

    Jibu

    Hiyo ni safii sana kwa kutujuza habari za muhumu kama hizi.

    Jibu

    Wakaze buti

    Jibu

    Safi kwa dondoo nzuri za kimichezoo.# meridianbettz.

    Jibu

    Jamv leo litakuwa poa

    Jibu

    Kweli inabidi wajipange, maana ngoma nzito.

    Jibu

    Mchezo mkali sana.

    Jibu

    huu mchezo unaweza ukawa na gg tu

    Jibu

    Ya leo Ndio ngumu kuelezeka kabisa maana wote ni mafundi

    Jibu

    mmh

    Jibu

    Ilikuwah bonge la derby thanks meridian kwa update

    Jibu

    Mechi ilikuwa ya kibabe sana

    Jibu

    Mechi ilikuwa Kali sana

    Jibu

    Kaz kaz

    Jibu

    Itakua hatariii

    Jibu

    hii game ya Leo itakua ngumu sana

    Jibu

    Maskini Frankfurt nawapenda#Meridianbettz

    Jibu

    Buyern atapata tena ushindi mwembamba

    Jibu

    Litakua bonge la mechi

    Jibu

    Kazi kazi

    Jibu

    itakuwa bonge la mechi#meridianbettz

    Jibu

    Nahisi mechi zote kuwa na magoli mengi #Meridianbettz

    Jibu

    Itakuwa bongee la mechiii.za kibabeee

    Jibu

    Ilikuwa bab kubwa Asante kwa mrejesho

    Jibu

    Duuuh

    Jibu

    Hatari sana

    Jibu

    Bayern Munich ushindi upo

    Jibu

    Hii mechi ilikuwa atarii sana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.