Meneja wa Leicester City, Brendan Rodgers anaamini James Maddison bado yupo katika nafasi ya kurejea kwenye fomu nzuri, wakati kukiwa na maswali juu ya fomu ya mchezaji huyo wa miaka 24.
Maddison, ambaye aliwasili kutoka Norwich City mwanzoni mwa msimu wa 2018-19, alifunga magoli saba na asisti saba kwenye msimu wake wa kwanza Uingereza, kabla ya kuongeza kuwa na magoli nane na asisti saba msimu uliopita.
Hata hivyo, staa huyu ameshindwa kuona lango kwa mechi 15 za mwisho za Leicester, pia licha ya kuanza katika michezo yao yote minne ya kwanza ya kampeni mpya, lakini Brendan Rodgers anaamini kiungo wake ataweza kurejea kwenye fomu.

“Kila mchezaji atapitia wakati fulani, haswa na kuwa bora kwa James katika miaka hii michache iliyopita. Katika kipindi cha miezi 12 hadi miezi 15, majeraha yamemrudisha nyuma zaidi ya kiwango chake halisi.”
“Kiwango alichokuwa nacho na kila mwanasoka ni kile kile, unapitia kipindi ambacho haufiki mwisho kabisa. Lakini sina shaka kwamba itakuwa kwa msimu wote , atarejea kwenye fomu yake na ataanza kuimarika, sio tu binafsi lakini kama timu, atarudisha fomu hiyo.”
Brendan Rodgers
Unaanzaje siku yako na kuimaliza bila kupitia katika kasino bomba za meridianbettz, mchezo mashuhuri wa Disco Funk unaweza kukufanya uwe mshindi leo hii.!


