Bruno Fernandes Atoaneno Kuhusu Penati

Waswahili husema ‘nabii hakubaliki nyumbani’. Ukitaja Bruno Fernandes ukiwa Ureno, sio wengi watakaoshtuka kama utakavyosema Cristiano Ronaldo. Ila mtaje Fernandes ukiwa Manchester na utapigiwa makofi kwa shangwe kubwa kutokana na uwezo wa kiungo huyo.

Bruno Fernandes afunguka kuhusu kumpatia Marcus Rashford penati licha ya kwamba ilikuwa ni nafasi yake kupachika ‘Hat-trick’ kwenye Ligi ya Mabingwa akiwa na Man United.

Mchezo wa 4 kwenye hatua ya makundi kunako Ligi ya Mabingwa, Man United walikutana na Istanbul Basaksehir katika mchezo wa marudiano baada ya kupoteza mchezo wa kwanza.

Alikuwa ni Bruno Fernandes aliyepeleka shangwe kwa mashabiki wa Manchester United baada ya kupachika magoli 2 ndani ya dakika 20 na mchezo ulimalizika kwa ushindi wa 4-1.

Fernandes amehusika kwenye magoli 34 (magoli 21 na pasi 13 za magoli) kati ya mechi 35 alizoitumikia Man United.

Bruno Fernandes alikuwa na nafasi ya kupachika goli la tatu lakini aliamua kumuachia Rashford jukumu la kupiga penati kunako dakika ya 35 na muingereza huyo hakufanya makosa, alipachika goli la 3.

Akizungumzia uamuzi huo, Fernandes amesema “ni kweli kila mchezaji anataka ‘hat-trick’ lakini baada ya mchezo wa EPL (dhidi ya West Brom) nilimwambia Rashford atapiga yeyote itakayofuata.

“Lakini pia ni miongoni mwa wafungaji bora wa Ligi ya Mabingwa kwa hiyo ni muhimu kwake kuendelea kujiamini zaidi.

“Haijalishi ni nani anapiga penati, kitu cha muhimu ni ushindi”

Kocha Ole Gunnar Solskjaer naye alikuwa na chakusema kuhusu uamuzi wa Fernandes. Ole amenukuliwa akisema “Marcus ni mpigaji mzuri wa penati na Bruno anajiamini sana, kama Bruno alitaka kumpatia Marcus sasa kwanini asifanye hivyo? Anthony Martial alipiga kwenye mechi dhidi ya Leipzig – sasa kwanini wasishirikiane?

Huu ni mchezo wa kwanza kwa United kuongoza kwa magoli 3 kabla ya mapumziko kwenye Ligi ya Mabingwa. Mara ya mwisho walifanya hivyo kwenye mchezo dhidi ya Roma (7-1) mwezi Aprili, 2007.


USICHELEWE KUKAMATA MKWANJA HUU!

Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.

Meridianbet Tanzania Casino

SOMA ZAIDI

26 Komentara

    fernandes yupo vizuri sana ata wasipomkubali kwao potelea pote sisis mashabiki tunaangalia ni nini anafanya

    Jibu

    Fernandes anastahili pongezi maana magoli 2 ndani ya dakika 20 si mchezo.

    Jibu

    Hatari san

    Jibu

    Fernandes anajua nini anafanya katika klabu yake ndiomaana man u wanamuamini sana

    Jibu

    Namkubali sana uyu jamaa Fernandes kwan anajua kulisakata soka vizuri tu

    Jibu

    Kitu muhimu in utendaji wa kazi

    Jibu

    Fernandes Yuko vizuri pongezi kwake

    Jibu

    Safi Fernandez

    Jibu

    Fernandez anajua nini anafanya..

    Jibu

    Vizur sana Fernandez

    Jibu

    Fernandez Yuko poa

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Fanya kwa nafas yako

    Jibu

    Sisi mashabiki tunakubali kazi yake kwenye mpira

    Jibu

    Fernandez ni mmoja wachezaj muhimu ndani ya manchester united hv sasa

    Jibu

    Vizuri sana

    Jibu

    Bruno amekua mtu makin na ameleta morali sana man u

    Jibu

    Nice upadate 👍

    Jibu

    Man U imekuwa ikipata penati karibia kila mchezo jambo ambalo linashangaza wengi. Bruno ni mpigaji mzuri wa Penati na alikuwa muungwana kumwachia mwenzie

    Jibu

    Nice

    Jibu

    Hatari yake.

    Jibu

    Kijana yupo vizuri

    Jibu

    Kijana anajua

    Jibu

    Yuko vizuri

    Jibu

    Bruno anajua bwana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.