Kila mtu ana mtu anayemkubali zaidi, na inapofika nafasi ya kufananisha watu wenye uwezo na historia katika soka kila mmoja huwa na maoni yake! Kwa Martin Cardetti, kama angekuwa na nafasi ya kuchagua, angemchagua Ronaldinho dhidi ya supastaa wa Barcelona Lionel Messi!
Ronaldinho alifurahia na kupeta sana enzi zake za soka alipokuwa Barcelona, Milan, PSG na pia Brazil. Alifanikiwa kushinda Ballon d’Or mwaka 2005, Kombe la Dunia, Ligi ya Mabingwa na LaLiga ikiwa ni baadhi ya mafanikio yake kwenye soka.
Messi kwa upande mwingine, naye anachukuliwa kama mwanasoka wa kipekee na mwenye uwezo mkubwa kuwahi kutokea kwenye soka. Ana rekodi ya kushinda Ballon d’Or mara 6, akiwa na mataji ya La Liga 10 kibindoni, pia ana medali 4 ya Ligi ya mabingwa na mataji mengine mengi!
Lionel Messi na Ronaldinho walipata nafasi ya kucheza pamoja Barcelona, na kama unakumbuka vyema wakiungana na Neymar waliitwa wazee wamaajabu wa 3 kutoka Barcelona!

Lakini kwa Cardetti, yeye anasema Ronaldinho ni mchezaji ambaye ameguswa na Mungu na kuwa na uwezo wa ajabu. Walikuwa timu klabu moja ya PSG kabla ya Ronaldinho kusepa kwenda Barcelona mwaka 2003.
Licha ya kutambua vyema mafanikio ya Messi, Cardetti yeye akiwa kama kocha angemchagua Ronaldinho kwa ubora dhidi ya Messi.
“Nilikuwa na Ronaldinho kwa mwaka mmoja, na ni mchezaji wa tofauti, ameguswa na mungu. Wakati wote alifurahia, akiwa na mpira alifanya vitu na kufanya mazoezi sana ili aweze kuonesha vitu hivyo kwenye mechi. Unamuona kuwanzia mazoezini, kwenye mechi na kila kitu anachokifanya anafanya tofauti na wengine.”
Cardetti anasisitiza kuwa yeye wachezaji wa aina ya Ronaldinho wanatokea mara chache sana kwenye historia ya soka, na anajivunia kuwa alikuwa karibu na mchezaji kama huyu. Ungekuwa wewe ni kocha, kati ya Messi na Ronaldinho nani angekufaa zaidi kwa uwezo wao? Achia komenti hapo chini


Ester jackson
Ronaldinho yuko juu
SADICK
Kwangu Messi ni zaidi ya yeyote
David Pere
Ronaldinho kwangu zaidi ya Messi sababu huyu jamaa Ndio mwalimu wa Messi,
Agness
Mesi ndio habari ya mjini
Warda
Ronaldinho mnyama
Gabriel
Gaucho mkali wao
Asha mvugalo
Fundi wa mpira
Njiku
Kipnd ronaldinho anafnya yke Messi alikuwa anatulia baada ya dinho kutoka Barcelona ndio Messi akapewa Jez ya dinho jamaa alikuwa kama Corona anatisha kwa kile kipnd
Daniel
Ronaldino was great, Messi is greater #meridianbettz
Furahav
Mess anajua.
Nasra
Messi kiungo
Hidaya Mohammed
Messi ndio mkali wao
Zeiyana iddi
Gaucho namkubali sana
felister
dhino kabali yao
Dorophina
Messi ndo baba lao
aisha
mesi mkali hana mpinzani
Neema hassan
Messi Hana mpinzan..
Neema juma
Messi mie namkubalii