Chan 2021: Tanzania Kuwanyamazisha Zambia

Kuelekea mashindano ya Chan 2021, Tanzania inaamini inauwezo wa kuwanyamazisha Zambia (Chipolopolo). Hii ni kwa mujibu wa Nadir Haroub “Cannavaro”.

Taifa Stars imepangwa kundi D kwenye mashindano ya Chan 2021 ambayo yatafanyika nchini Cameroon. Stars wataitupa karata ya kwanza siku ya Jumanne dhidi ya Zambia katika dimba la Limbe Omnisport.

Kuelekea mchezo huo, Stars wanaamini wanakila silaha ya kuwaangamiza Zambia ambayo inafundishwa na kocha Milutin ‘Micho’ Sredojevic. Imani hii ni baada ya Tanzania kudai wanazifahamu mbinu na namna ya uchezaji kwa timu yeyote iliyochini ya Micho.

Taifa Stars wakiwa mazoezini.

Micho anahistoria ya kuvifundisha vilabu mbalimbali vya ukanda wa Afrika Mashariki na hii inawapa nguvu Stars kwa kuwa wanamfahamu vizuri katika ubora wake wa kuandaa timu.

Kwa mujibu wa Cannavaro ambaye aliwahi kuwa mchezaji wa Stars na sasa ni meneja wa kikosi hicho amesema, “ninamfahamu vizuri Micho. Alishawahi kunifundisha na ni kati ya makocha wanaotumia sana viungo. Timu yake inajengwa na viungo na anauzoefu wa kufundisha timu nyingi za Afrika Mashariki.

“lakini pia ninajua tunakocha mzuri, ameangalia video za namna Zambia inavyocheza na tutajipanga vizuri kupambana naye, tutajaribu kuzuia namna ya uchezaji wake, tunajua inawezekana.”


USHINDI UPI NI MKUBWA KWAKO, £2,000,000? 🤑

Pokea mualiko wa Meridianbet na Pragmatic Play kutengeneza mkwanja kwenye kasino ya mtandaoni sasa. Jiunge sasa kupata ishindi huu.

INGIA MCHEZONI

16 Komentara

    Wajipange wasije kujikuta wao ndiyo
    Wanaenda kupigwa

    Jibu

    Sawa sie tunataka ushindi tu

    Jibu

    Cha msingi ni kujipanga watawaangusha tu

    Jibu

    Tanzania waongeze juhudi za kutosha ili wasonge mbali

    Jibu

    Tanzania lazima amgalagaze mtu

    Jibu

    Vizuli tanzania sisi tunataka ushindi

    Jibu

    Kila la her kwao

    Jibu

    ushindi lazima

    Jibu

    Kila la kheri

    Jibu

    Kazi kazi, Kila la kheri Tifa Stars

    Jibu

    Kombe let tz

    Jibu

    Kila kheri Tz

    Jibu

    Kila la kheri timu yetu yataifa

    Jibu

    TZ sio watu wamasiaraa aiseee

    Jibu

    Kila LA kher Taifa stars

    Jibu

    Watajua hawajui

    Jibu

Acha ujumbe