Ushindi wa ugenini wa magoli mawili kwa moja, dimbani Villa Park umewahakikishia Chelsea kusalia salama katika nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo huku wakiwa na alama tano zaidi ya Manchester United wanaoshika nafasi ya nne.
Magoli mawili ya Christian Pulisic na Olivier Giroud yaliwahakikishia usalama vijana hao wa Frank Lampard katika nafasi ya nne huku yakiongeza matumaini yao ya kushiriki Champions League msimu ujao.
Matokeo hayo, kwa upande mwingine yamezidi kudidimiza juhudi za Aston Villa ambao wanapigania kubaki katika ligi kuu msimu huu. Ilikuwa ni nafasi nzuri kwa timu hiyo kujiondoa katika hatari ya kushuka daraja hasa baada ya timu za West Ham na Bournemouth ambazo nazo zinapambana kubaki ligi kuu kupoteza katika michezo yake ya Jumamosi.
Aston Villa walikuwa wa kwanza kupata goli katika mchezo huo. Goli hilo lilifungwa na Kortney Hause katika dakika ya 42 tu ya mchezo na kuwafanya waende mapumziko wakiwa kifua mbele.
Hata hivyo bahati haikuwa upande wao kwani Chelsea walitumia vizuri udhaifu wa Aston Villa wa kujilinda zaidi kuliko kushambulia kuwaadhibu.
Kwa matokeo hayo, Chelsea wanazidi kujiwekea mizizi katika nafasi ya nne wakiwa na alama zao 51 huku Aston Villa wakishuka mpaka nafasi ya 19 wakiwa wamejikusanyia alama 26 katika jumla ya michezo 30!


Ester jackson
Safii sana Chelsea jembe langu kwa kujitahiji kubaki katika nafasi ya nne hivyo mnazidi kutupa mashabiki wenu nguvu mpya sasa kweli tangu mtoke katika kipindi kigumu cha corona mko vizuri sana
warda
Wanabahati sana ilikuwa bado kidogo tu watoke sare#Meridianbettz
Gabriel
Chelsea wamepanda sana msimu huu mpak kufikia nafas ya nne iko poa sana na kuwaacha Manchester United kwa alama tano hivyo mechi ijayo akishinda atakuwa katika nafasi nzur sana
Kwa upande wa Aston villa msimu huu wanaonekana hawako vzur sana
Maana mchezo uliopita mpaka
Kuwafanya watoke suluhu
wanajikuta wapo katika wakati
mgumu sana
# meridianbet Tanzania
Njiku
Yalikuwa matokeo mazuri kwa chelsea kupata arama tatu na kujikita na kukaa katika nafasi ya nne wakifuatiwa na man u tafauti ya arama tano ipo safii kabisa ila mbaya kwa aston villa maana watashuka daraja kipigo hicho kinafanya kukaa kwenye nafasi mbaya zaid,champions ship inawahusu dah mtanzania mwenzetu bora angebaki gent ila sio mbaya labda atapata timu nyngine mchawi dua tu
Zeiyana
Matokea mazuri kwa Chelsea kupata arama ya tatu na kuwa katika nafasi ya nne mnazidi kuwapa moyo mashabikj wenu
Omary lukumbi
Pongez kwa Chelsea kuendelea kujikita nafasi ya nne ila waendeleze hvyo hvyo moto mpk mwisho wa msimu maana huyo alioko chini yake anaitaman hyo nafasi kwa hamu sana
Povel
Kwl kwa upande fulan Chelsea imewavusha kuongezah gepu la point kwny mbio za top 4 ingawah Aston villa samata timu inazid kwenda chn Ila kwny foot ball hakuna huruma ndo mchezo wenye matokeo ya kikatil sana sema Aston villa nafas ipo iliwawez kupgana kutoshuka daraja na Chelsea nafasi wanayo kupambana top 4 thnks meridian bet tz kwa update za michezo
isha
Pongezi kubwa kwa chelsea ila msibweteke
Amiri Kayera
Aston villa Bax wajipange championship Tu
Tahiya
Jahazi linaenda kuzama Aston Villa kiu ya watanzania kumtazama Samatta inapotea
felister
habari njema kwa mashabiki wa chelsea
Issa
Villa walishindwa kiendeleza jihad yao kwenye hii mechi lakini uzoefu na umahiriwa chelsea uliwafanya waondoke na pointi 3
Shafii
Mi naamini kwenye ligi yeyote kila mmoja anaangalia nafasi yake
Edgar
ni kweli matoke mazr ya mchezo kati yake na astonivilla
tumaini
Maoni:hali sio nzuri kwa Aston villa
Furahav
Chelsea wako vizuri.
Mwanaidi
Chelsea hongera sana ila muendelee kukaza msiwe wazembe
Cathe
Hongera wapo nafasi nzur katika msimamo wa ligi ila astonvilla wanapumulia mashine maskin samatta
Mwajuma
Katika mechi hii Chelsea walipindua meza kibabe sana hongera kwao
Hamidu
Team samata ! mtu samehe kwa kweli sioni kabisa Kama Aston villa itabaki EPL
Jullie
hao ndo blue
Sabrina
Maoni:Hongera sn chelsea mko vzur
Hidaya
The blues endeleeni kunipa raha
Theckla
Aston Villa amekalia kuti kavu
Zuhura omary kindamba
Chelseawako vizuri sana ila Aston villa wasikate tamaa kwa ilo wanatakiwa kujipanga kwa upya katoka msimu wa ligi
fatumakasomo
Hongera sana Chelsea kujikita nafasi ya4 waendelee ivo ivo
Theonestina
Pongezi ziende kwa Chelsea
Aziza mushi
Pongezii kwa Chelsea 👏
Samiah
Pongezi kwao chelsea
Evaluziga
Chelsea wako vizuri
mwakalosi
dah dua imekataa United bado hali mbaya
Rehema
Chelsea wako vizur wakaze buti ongera zao
Saupha mohamed
Chelsea imejitaidi waendelee kukaza butii wadiludi nyuma
Leonard
Astonvila njia ya kushuka daraja nyeupe
Elika
Chelsea wako vizur kwa sasa
Mwanahamisi
Chelsea wako vizuri
Antony Luseno
Hili lilikuwa wazi kwamba Chelsea lazima ashinde
Neema juma
Heshima kwenu Chelsea
Magdalena
Hongera sana Chelsea mmejitahidi Sana na mumeoneaha juhudi mpaka kufika nafasi ya nne
Caroline
Chelsea wanaweza kuchukua ubingwa
Dorophina
Hongera kwao Chelsea mpira ulikuwa mzuri htr vikosi vilijiandaa vzr
Khadija
Chelsea wanaweza kuchukua ubingwa#meridianbettz
Genia Sikaluzwe
Chelsea wamejipanga vizuri Sana
Salma
Chelsea nyota bahati iko upandea wao
Amani
mbaya kwa aston villa maana watashuka daraja kipigo hicho kinafanya kukaa kwenye nafasi mbaya zaid,champions ship inawahusu dah mtanzania mwenzetu bora angebaki genk Ila akuna kufeli#meridianbettz
Isaya massawe
Aston Vila kazi hana
David Pere
Kweli hawajafanyia haki jamanii
Sadick
Vita iliyopo kwa timu zilizohatarini kushuka daraja kujiokoa na timu zinazotaka tiketi ya kucheza UEFA CHAMPIONS LEAGUE#meridianbettz
Devotha
Namuona samatta akicheza championship
farida ahmadi
Hongera Sana Chelsea kwa kubaki nafasi ya nne na hata pia Aston vila pia nao wasikate tamaa waendelee kukaza buti
Mariam mtandama
Duuuh kweli hawajamfayia haki
Hope mwaikuka
Ze blues
Ernest
Sam Magoli amekwenda Uingereza kwenye wakati mbaya sana kwani itakuwa vigumu kumuona akilisakata soka kwenye ligi kuu ya uingereza hasa ukiangalia hali mbaya kwa Villa
Latifa juma mohamed
Gudaguda Chelsea kwa kuongeza point tatu tunatarajia mazur Zaid yajayo
Agness
Chelsea wako vizuri Sana
Angelina
Chelsea ni timu nzuri na inawechezaji wazuri
Lydia Emmanuel Magoti
Chelsea wapo vizuri
Emmy cleopa
Chelsea wanafanya vizuri
Christa
Jamani samatta wetu dahhhj
Asia Abdy
Chelsea tuko vizurii