COVID-19 Kuwaeka Nje Dyche na Pep.

Maambukizi ya COVID-19 yanaendelea kuwatesa watu duniani. Kwenye ulimwengu wa michezo, hiki ni kikwazo kikubwa kwa sasa.

Nchini Uingereza, takribani michezo 17 ya Ligi kuu imeshaghairishwa tokea mwanzoni mwa mwezi Disemba mpaka sasa. Na bado, huenda kukawa na muendelezo wa michezo kughairishwa kwa sababu zinazohusiana na COVID-19.

Kuelekea michezo ya hatua ya 3 ya Kombe la FA, Kocha wa Burnley, Sean Dyche na kocha wa Man City, Pep Guardiola, watakosekana viwanjani baada ya kukutwa na maambukizi ya virusi hivyo.

Kwa Burnley, tayar wanamichezo 3 ambayo imeshaghairishwa mpaka sasa. City ndio timu pekee ambayo haijakumbana na dhoruba la mchezo wake kughairishwa mpaka sasa. Lakini, imeripotiwa kuwa, Man City wanajumla ya watu 21 (wachezaji na wafanyakazi) ambao wameathirika. Miongoni mwao ni Pep Gurdiola na msaidizi wake, Juanma Lillo.

Kutokana na hali ilivyo, kocha msaidizi, Rodolfo Borrell, ataiongoza Man City kwenye mchezo dhidi ya  Swindon huku Sean Dyche pia akiendelea kukaa karantini na kuwakosa Huddersfield.


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.