Cristiano Ronaldo alichapisha picha akifanya mazoezi mara tu baada ya droo ya hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa ilipofikia tamati siku ya Alhamisi.

Mshambuliaji huyo wa Manchester United alinukuu chapisho lake kwenye Twitter: “Endelea kufanya kazi na kuzingatia” pale tu timu 32 zilipojua hatima ya mashindano ya klabu bingwa barani Ulaya, ambayo huenda hayatakuwa na Ronaldo.

Inaonekana Ligi ya Mabingwa itamkosa mfungaji bora wa muda wote kwa mara ya kwanza tangu 2003 baada ya United kushindwa kumaliza kwenye nafasi nne za juu msimu uliomalizika ili kuifanya timu hiyo kushiriki michuano ya mabingwa wa ulaya.

Mashetani Wekundu waliweka rekodi mbaya zaidi kuwahi kutokea katika ligi kuu msimu uliopita chini ya Ole Gunnar Solskjaer na Ralf Rangnick, wakimaliza nafasi ya sita kwenye jedwali licha ya kurejea kwa Ronaldo.

