Mshambuliaji wa zamani wa Juventus, Athletic Bilbao na Uhispania Fernando Llorente amestaafu kucheza soka akiwa na umri wa miaka 37.

Llorente ambaye amekuwa bila klabu tangu mwisho wa msimu uliopita alitangaza kwa Movistar Plus, kuthibitisha mwisho wa kazi yake ya juu ya miaka 18.
Alipoulizwa kuhusu kuendelea kucheza soka, alijibu “Hapana” na kupendekeza badala yake “atajiweka fiti kwa michezo mingine. Fernando alianza maisha yake ya soka akiwa na Athletic, ambapo alicheza kwa misimu tisa kwenye kikosi cha kwanza, akifunga mabao 84 katika michezo 262 ya LaLiga.
Kisha akahamia kwa wababe wa Serie A Juventus, ambapo alifunga mabao 16 katika mechi 34 za ligi katika msimu wake wa kwanza, ingawa hakuweza kurudia kiwango hicho kabla ya kuondoka kwa uhamisho wa bure na kurejea Uhispania na Sevilla mnamo 2015.

Baada ya msimu mmoja kwenye Uwanja wa Ramon Sanchez Pizjuan, ambapo alifunga mabao manne pekee katika mechi 23 za LaLiga lakini akashinda Ligi ya Europa, Fernando alihamia Ligi Kuu akiwa na Swansea City.
Alifunga mabao 15 ya ligi katika mechi 33 akiwa na Swans kabla ya kutimkia Tottenham baada ya mwaka mzuri huko Wales. Llorente alitatizika kwa muda wa mechi akiwa Spurs, ingawa, Harry Kane ndiye mshambuliaji mahiri katika klabu hiyo.
Walakini, alichukua jukumu muhimu katika mbio zao za fainali ya Ligi ya Mabingwa 2019, akifunga bao lililoifanya Spurs kutinga nusu-fainali kwa gharama ya Manchester City.

Llorente hakuweza kurejea katika ubora wake wa awali alipokuwa Napoli au Udinese, kabla ya kucheza ule uliokuwa msimu wake wa mwisho kurejea Uhispania akiwa na Eibar katika Kitengo cha Segunda.
Alishinda mataji matatu ya Serie A, mataji mawili ya Coppa Italia na Ligi ya Europa wakati wa maisha yake ya kilabu. Llorente pia alikuwa sehemu ya kikosi cha Uhispania kilichoshinda Kombe la Dunia la 2010 na Euro 2012, akiichezea nchi yake mechi 24 kwa jumla, akifunga mabao saba.

