Kiungo wa klabu ya PSG Xavi Simons amefanikiwa kujiunga na klabu ya Rb Leipzig kwa mkataba wa mwaka mmoja ukiwa wa mkopo mpaka mwezi Juni 2024.
Xavi Simons amejiunga na Rb Leipzig akitokea klabu ya Psv Eindhoven kwa mkopo wa mwaka mmoja, Hivo PSG imeendelea kumtoa kwa mkopo kinda huyo wa miaka 20 ili aweze kupata muda wa kucheza zaidi kwajili ya matumizi ya baadae.
PSG inamtoa kijana huyo kwa mkopo kwajili ya kuweza kupata nafasi ya kucheza zaidi ili apate ukomavu ambapo watamuhitaji baadae ili kuja kuimarisha kikosi chao miaka ya mbeleni ambayo atakua ameshapata uzoefu wa kutosha.
Xavi Simons amekua na kiwango bora sana ndani ya klabu ya PSV ya nchini Uholanzi na kua moja ya wachezaji waliofanya vizuri sana ndani ya ligi kuu ya Uholanzi Eredivise.
Rb Leipzig ni wazi wamepata mchezaji mwenye uwezo mkubwa ambaye atakwenda kuimarisha safu ya kiungo ya klabu hiyo msimu ujao, Kwani Xavi Simons anazungumzwa kama moja ya vijana wanaofanya vizuri zaidi kwenye soka barani ulaya kwasasa.

