Mashindano ya kimataifa kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani barani Afrika, Chan. Yamemalizika wikiendi hii.
Timu ya Taifa ya Morocco imeweka historia ya kuibuka kidedea mara mbili mfululizo kwenye mashindano hayo.
Morocco waliingia kwenye mashindano haya kama mabingwa watetezi baada ya kuibuka kidedea msimu uliopita. Japo walianza kwa kasi ndogo, mambo yalikuwa tofauti kwenye michezo yao ya mwisho kwenye hatua ya makundi.
Morocco alikuwa kundi moja na Togo, Rwanda pamoja na Uganda. Alishinda 1-0 dhidi ya Togo, akatoka suluhu na Rwanda kabla ya kuwagaragaza Uganda 5-2.

Katika hatua ya robo na nusu fainali, The Atlas Lions waliwaburuza Zambia na Cameroon kabla ya kuwafata Mali kwenye hatua ya fainali kwa mwaka 2021.
Magoli ya Soufiane Rahimi na El Kaabi yalitosha kuwapa ubingwa Morocco ambapo pia – Rahimi amemaliza mashindano haya kama mfungaji bora (magoli 5) na mchezaji bora wa mashindano ya Chan 2021.
Hakuna timu iliyowahi kutetea ubingwa wa mashindano haya tangu kuanzishwa kwake, hii ni mara ya kwanza Morocco wamefanya hivi na wameweka rekodi hii.
Unaweza kuvuna mkwanja mrefu kadiri uwezavyo kupitia mchezo wa Gold n Rocks kwenye kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Ni rahisi! Vigezo na masharti, kuzingatiwa.



warda
Hongera yao Najua mwaka Mwingine Tanzania tutashinda tu
Khadija
Hongera yao
Venerose
Hongereni sana
Rahma
Hongera zao
Hopemwaikuka
Congratulations to them
Sarah
Ongera kwao
Dorophina
Pongezi kwao morocco
Magdalena
Safi Sana Morocco
Angelina
Safi
Ernest Kimeru
Sasa Morocco hawana mpinzani
Mwanahamisi
Pongezi kwao
Sania
Morocco wapo juu
lombo
habar njema
Lydia Emmanuel Magoti
Habari nzuri
Ester mmakasa
Wako vizuri safari hii.