Everton wamesema “wameshtushwa” baada ya picha kusambaa zikimuonyesha straika wake Moise Kean akiwa kwenye party ya nyumbani.
Ripoti zinasema Muitaliano huyo alijichukua video mwenyewe wakati wa party akiwa kwenye nyumba yake.
Everton wamekiri “wameshtushwa kuona mchezaji wa timu ya wakubwa kukiuka maagizo ya serikali na sera za klabu kuhusu Corona. Tumesikitishwa sana na kitendo cha mchezaji wetu.”
Kwenye taarifa yao, Everton wameongeza: “Everton siku zote imekuwa na utaratibu wakufuata maagizo ya serikali – ikiwemo sheria na ushauri wa ndani au nje ya nyumbani kwa kutumia mfumo rasmi wa mawasiliano ili kuwapa taarifa watumishi wake ikiwemo wachezaji.
“Mashujaa wa NHS wanatakiwa waheshimiwe kwa kazi ngumu na kijitoa. Njia nzuri ya kuwaheshimu ni kufanya yale wanayoshauri kijilinda.”
Hadi Jumaosi jioni watu 20000 walifariki kwa virusi vya Corona katika Hospital za UK, takiwimu kutoka Kitengo cha Afya.
Kean – alisajiliwa na Everton kutoka Mabingwa wa Italia Juventus kwa dau la £25.1m kipindi cha majira ya kiangazi – ni mchezaji wa EPL aliyevunja sheria za kukaa nyumbani hivi karibuni baada ya Kyle Walker, Serge Aurier na Moussa Sissoko
Zeiyana
Mungu pekee ndio hanaweza kutuondosha na janga hili