PSG Yamuwinda Joao Neves
Makala iliyopita
Nuri Sahin Kocha Mpya Borussia Dortmund
Makala ijayo
Lautaro Martinez Mbioni Kusaini Mkataba Mpya Inter
Klabu ya Benfica inasema haimuachii kiungo huyo chini ya ada ya uhamisho ya €120 milioni jambo ambalo limewafanya vilabu vingine kama Arsenal na Man United ambao wamekua wakimfukuzia kutulia kwanza, Klabu ya Benfica miaka ya hivi karibuni wamekua wakifanya biashara yenye faida kubwa sana wakiuza wachezaji chini ya Rais wa klabu hiyo Manuel Rui Costa.
Mpaka sasa inaonekana mwenye kisu kikali ndio atakula nyama kwa maana ya kwamba klabu ambayo itatoa dau nono ambalo wanataka klabu ya Benfica ndio watapata saini ya kiungo huyo, Kwani vilabu kama Man United, Arsenal, PSG ambao waingia kwenye mbio hivi karibuni wanaitaka saini ya kiungo huyo mwenye ubora mkubwa.