Manchester City wamemrudisha Aro Muric mwenye miaka 19, aliyekuwa NAC Breda kwa mkopo kutokana na jeraha la Bravo ambaye anahofiwa kuwa jeraha lake litaendelea kuwa kikwazo. Bravo ambaye alipata jeraha kwenye sehemu ya chini, nyuma ya mguu wake wakati akiwa mazoezini anatarajiwa kusafiri kwenda Barcelona leo kwa ajili ya vipimo zaidi.
Bravo mwenye umri wa miaka 35 aliposti katika ukurasa wake wa instagram akizungumza kwa hisia juu ya kurudi kwake huku akisisitiza kuwa yeye huangalia zaidi upande chanya wa mambo, na namna ujasiri unavyohitajika kila mahali.
Golia anayetegemewa zaidi baada ya Bravo kupata jeraha ni Ederson, Lakini Muric ambaye ameonekana mara moja mchezoni kule NAC Breda alikokuwa kwa mkopo ataungana na Grimshaw ambaye kumpa nafasi pep Guardiola kuchgagua.


isha
Pole sana bravo
Povel
Gud news