Ripoti zinadai kuwa Real Betis wametoa ofa rasmi kwa Manchester city kumchukua Oleksandr Zinchenko kwa mkopo huku wakifikiria kumchukua moja kwa moja. Chanzo cha habari cha kihispania Mundo Deportivo kinaripoti kuwa Mancity kwa sasa wako kwenye mazungumzo na betis na huenda wakakubali ofa hiyo na kumchukua Oleksandr Zinchenko kwa mkopo ambaye anaweza kuchukuliwa moja kwa moja kwa thamani ya Euro milioni 12 hadi juni 2019 kwa kulipa kwa vipindi vitatu .
Oleksandr Zinchenko anaaminika kuwa kijana mwenye kipaji cha pekee cha kucheza kama kiungo wa kati na pia kama winga, huenda mancity wakamchukua kijana huyu mwenye umri wa miaka 21. kutokana na taarifa yaMundo Deportivo mazungumzo yamepiga hatua kubwa ya makubaliano hivyo kutoa uwezekano mkubwa wa kijana kwenda Manhester City.


lombo
habari njema
Povel
Habar njema