Salah Asaidia Kijijini Kwao

Nyota wa Liverpool Mohamed Salah ametoa maelfu ya tani za chakula na nyama safi kusaidia wakazi katika kijiji chake cha nyumbani kwao huko Misri wakati huu wa janga la coronavirus.

Salah alituma vifaa hivyo katika kijiji chake cha Nagrig, karibu na mji wa Basyoun kaskazini mwa nchi, na pia Alituma ushauri wa jinsi ya kujiweka salama. Kijiji hicho kina wakazi zaidi ya 8500.

Baba wa mchezaji Huyo, Salah Ghaly, aliliambia gazeti la Al-Masry Al-Youm kwamba mtoto wake anatamani afya na usalama wa kijiji hicho, huku akiwataka wakazi waache mikutano mikubwa.

Aliongeza kuwa kijiji kimepatiwa Sanitizer na masks ambazo zinatarajia kusambazwa kwa wakazi kwa nia ya kupambana na kuenea kwa COVID-19, ambavyo vimesababisha vifo vya watu 205 nchini Misri.

Baba yake huyo aliongezea kuwa ng’ombe wawili watachinjwa na nyama hiyo itapelekwa kwa watu wa Nagrig na vijiji vinavyozunguka eneo hilo.

Mshambuliaji wa Liverpool Mohamed Salah alichapisha video ya Instagram akifanya mazoezi binafsi ambako yupo kizuizini nyumbani kwao akisubiri kuanza tena kwa soka huko England. Salah, ni kama wachezaji wote wa Premier League, wamekuwa wakijaribu kujifua ili kutunza viwango vyao na kuweka afya zao sawa..

2 Komentara

    Jambo zuri

    Jibu

    Mambo mazur

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.