Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ufaransa Kylian Mbappe ambaye kwasasa ni mchezaji wa klabu ya Real Madrid Kylian Mbappe kutambulishwa Jumanne ya tarehe 16 mwezi pale Santiago Bernabeu.
Mbappe atatambulishwa katika dimba la Santiago Bernabeu kama magwiji waliopita klabuni hapo walivyotambulishwa, Siku ya Jumanne itakua ni siku ya sikukuu kwa mashabki wa Real Madrid kwani wataenda kumuona mchezaji wao waliomsubiri kwa takribani miaka minne.Staa huyo wa kimataifa wa Ufaransa anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka mitano wa kuitumikia klabu ya Real Madrid kwa maana atakua klabuni hapo mpaka mwaka 2029, Lakini pia mabingwa hao wa ulaya watakua na uwezo wa kuendelea kua nae zaidi kama watahitaji kumuongezea mkataba.
Kinachosubiriwa kwa hamu zaidi ni kuona kama mshambuliaji Kylian Mbappe ataweza kuvunja rekodi ya Cristiano Ronaldo, Ambaye aliweka rekodi ya utambulisho wake kuhudhuriwa na watu wengi zaidi sasa Jumanne ndio inaweza kua siku ya rekodi kuvunjwa au ikaendelea kubaki hai.Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa anatarajiwa kuongoza safu ya ushambuliaji ya Real Madrid kuelekea msimu ujao akishirikiana na raia wa wawili wa kimataifa wa Brazil Vinicius Jr pamoja na Rodrygo Goes, Huku kitendawili kikiendelea kubaki kati yake na Vinicius Jr nani atacheza upande wa kushoto.
This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.
Strictly Necessary Cookies
Strictly Necessary Cookie should be enabled at all times so that we can save your preferences for cookie settings.
If you disable this cookie, we will not be able to save your preferences. This means that every time you visit this website you will need to enable or disable cookies again.