Juventus na Barcelona Zinamuwinda Jorginho

Ripoti mbalimbali zinasema kuwa klabu ya Juventus ya Italia na Barcelona ya Uhispania wanajipanga kwa ajili ya vita ya Januari kwa Jorginho, ambaye anaonekana kuwa njiani kuondoka Chelsea.

 

Juventus na Barcelona Zinamuwinda Jorginho

Mchezaji huyo wa Kiitaliano na Brazil mwenye umri wa miaka 30 amekuwa na The Blues kwa miaka minne sasa, akijiunga na klabu hiyo msimu wa joto wa 2018 pamoja na Maurizio Sarri.

Jorginho amethibitisha kuwa kiungo muhimu kwa Chelsea kwa miaka michache iliyopita lakini muda wake kwenye Ligi Kuu unaonekana kukaribia mwisho.

Na jarida la Sport la Uhispania, linasema kuwa mkataba wa Jorginho na Chelsea unaisha mnamo Juni mwaka ujao na klabu hiyo haina mpango wa kumpa mkataba mpya, hivyo kumaanisha kwamba anatarajiwa kuondoka katika miezi ijayo.

Juventus na Barcelona Zinamuwinda Jorginho

Juventus na Barcelona wote wana nia ya kumnasa kiungo huyo na Bianconeri wanaonekana kuwa na faida, kwa kuweza kumpa mchezaji huyo mshahara mkubwa. Jorginho amefunga mabao matatu katika mechi 18 katika michuano yote msimu huu akiwa na Chelsea.


AVIATOR

Ulishawahi kuwaza kuwa rubani wa maisha yako!! Kuwa rubani wa mchezo pendwa wa Aviator wa kasino mtandaoni. Aviator bonanza inazidi kutoa michongo ya mkwanja kwenye nyumba ya mabingwa. Unarusha ndege yako na unashinda, kuwa rubani wa kujivunia kwa kuibuka na mkwanja leo.

BONYEZA HAPA

Acha ujumbe