Klabu ya Manchester United wanaripotiwa kuwa wameamua kumchagua mchezaji mwingine atakayechukua nafasi ya Valencia kama nahodha wa klabu hiyo ikiwa nyota huyo atasepa klabuni hapo. Nani atauvaa ukepteni?
Taarifa zinadai kuwa nyota huyu anatarajiwa kusepa mwisho wa msimu huu baada ya kutumia miaka 10 klabuni hapo mkataba wake ukiwa unaisha msimu huu wa joto.

Taarifa pia zinataja kuwa nyota Paul Pogba yupo kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuchukua nafasi hiyo kwa kipindi hiki. Kwa mujibu wa ripoti ya The Sun, Pogba ameonesha uwezo mkubwa wa uongozi kwa kipindi chote alichokuwa chini ya Ole Gunnar na anaaminika zaidi na meneja huyu tofauti na ilivyokuwa kipindi cha Mourinho.
Hata hivyo inasemekana mambo yanaweza kubadilika kama Bosi Ole Gunnar atafeli kupata kibarua cha kudumu klabuni hapo. Pogba anatarajia kuongeza idadi yake ya magoli 11 klabuni hapo pindi atakapoingia kukipiga dhidi ya Southampton.

Kwanini Valencia anasepa?
Kwa mujibu wa ripoti jitihada za kufikia muafaka wa mazungumzo ya mkataba mpya wa nyota huyu zimegonga mwamba wakati staa huyu akiwa amebaikiwa na gemu kadhaa tu klabuni hapo hadi kumaliza msimu huu ambapo ndiyo mkataba wake unapooisha. Nyota huyu ataondoka kama mchezaji huru klabuni hapo.


Furahav
Daah akiondoka litakuwa bonge la pengo.
Povel
Valencia utakuwah pengo kubwa sana