Willian Atamani Kubaki Uingereza

Willian amesema anahitaji kubaki Ligi kuu ya Uingereza kama mkataba wake na Chelsea ukiisha majira ya joto.

Mbrazili huyo ameshindwa kufikia makubaliano na Chelsea, na ameongeza kuwa majadiliano “yamesimama”.

Arsenal na Tottenham wameonyesha nia ya kuhutaji huduma ya winga huyo wa Brazil.

Willian akisalmiana na Mourinho wakati akiwa kocha Chelsea

“Natamani kubaki Ligi Kuu ya Uingereza, lakini sio nakataa kucheza ligi zingine,” amesema Willian. Nitacheza mpaka mwisho wa msimu alafu tutaangalia nini kitatokea. Nimezoea maisha ya Uingereza. Sifikirii kurudi Corinthians kwasasa. Lengo langu ni kubaki Ulaya.”

Willian ameongeza: “Nahisi nipo kwenye ubora wangu wakati huu. Wachezaji wakuwa vizuri wakicheza na nadhani niko vizuri sasa.”

Akijiunga na Tottenham tutaona Willian akiwa pamoja na kocha wake wa zamani Jose Mourinho.

“Tuko vizuri na Mourinho, nimejifunza nikiwa chini yake na tumebaki marafiki,” amesema Willian. Bado tunawasiliana sana, lakini hatujaonana hivi karibuni. Sijamuona tangu arejee London.”

2 Komentara

    Baki tu hapo.

    Jibu

    Gud news

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.