Kaka Amesisitiza Kuwa Brazil Inaweza Kustahimili Bila Neymar

Kaka anaamini kuwa Brazil bado inaweza kufanya vyema katika Kombe la Dunia 2022, licha ya mchezaji nyota wa Taifa hilo Neymar.

 

Kaka Amesisitiza Kuwa Brazil Inaweza Kustahimili Bila Neymar

Mshambuliaji huyo wa Paris Saint-Germain,alishindwa kuendelea na mchezo na kutoka nje akichechemea katika dakika ya 80 ya ushindi wa Brazil 2-0 dhidi ya Serbia kwenye mchezo wao wa ufunguzi Kombe la Dunia.

Neymar mwenye umri wa miaka 30 alipata jeraha kwenye kifundo cha mguu wa kulia, huku akionyesha jinsi mguu ulivyovimba kwenye akaunti yake rasmi ya Instagram siku ya Jumamosi.

Kaka alikuwa miongoni mwa timu ya Brazili iliyoshabikiwa sana kwenye Kombe la Dunia la 2006. Lakini licha ya kujivunia pia mastaa kama Ronaldo, Ronaldinho na Adriano, Selecao walishindwa kutimiza matarajio na wakasonga mbele katika robo fainali kufuatia kipigo cha 1-0 kutoka kwa Ufaransa.

Kaka Amesisitiza Kuwa Brazil Inaweza Kustahimili Bila Neymar

Lakini miaka 16 mbele, Kaka ambaye ni kiungo wa zamani wa Milan na Real Madrid ana imani Taifa lake lina uwezo wa kufika mbali, hata Neymar akiwa nje ya uwanja, na amesema kuwa;

“Nadhani sasa, tunachoweza kuona kutoka Brazil, wana kundi lenye nguvu licha ya kumkosa Neymar lakini bado wana kundi kali sana katika Kombe la Dunia kwani unahitaji kundi imara sana hauhitaji baadhi ya wachezaji, mtu binafsi, bali unahitaji kundi lenye nguvu sana.”

Tangu alipocheza mechi yake ya kwanza ya Kombe la Dunia dhidi ya Croatia mwaka 2014, Neymar ameshiriki katika mechi 11 kati ya 13 za Brazil kwenye fainali hizo. Kipigo pekee cha Selecao akiwa naye kikosini kilitokana na kushindwa kwa robo fainali ya 2018 na Ubelgiji.

Kaka Amesisitiza Kuwa Brazil Inaweza Kustahimili Bila Neymar

Bila yeye, Brazil ilipoteza mechi zote mbili alipokosekana miaka minane iliyopita baada ya kupata jeraha baya la mgongo dhidi ya Colombia, walipata aibu ya kufungwa mabao 7-1 katika nusu fainali dhidi ya Ujerumani, kabla ya kufungwa 3-0 na Uholanzi katika mchezo wa kuwania nafasi ya tatu.


Je wewe hucheza Kasino Mtandaoni na umekuwa ukijiuliza ni mchezo gani rahisi na mzuri kwa ushindi? Basi Usihangaike Aviator ni rahisi zaidi kucheza na kushinda, kingine cha zaidi ni kwamba Aviator Bonanza imerudi tena Cheza zaidi ujiweke kwenye nafasi ya kushinda Samsung A23.

BONYEZA HAPA KUCHEZA

 

 

onana

Acha ujumbe