Staa wa timu ya taifa ya Brazil Neymar Jr ana uwezekano mkubwa wa kukosa mechi za kombe la dunia zilizobakia kutokana na majeraha aliyoyapata.
Neymar aliumia katika mchezo wa kwanza wa wa makundi waliocheza na timu ya taifa ya Serbia ambapo alionekana kupata maumivu ya enka na kukosekana katika michezo miwili iliyobakia ya hatua ya makundi ambapo Brazil ilishinda mmoja na kupoteza mmoja.
Mchezaji huyo ambaye alionekana kama atarejea punde tu baada ya hatua ya makundi ya michuano hiyo kumalizika lakini taarifa zinaeleza mchezaji huyo ana hatihati ya kukosekana kwenye michezo iliyobakia ya timu ya taifa ya Brazil.
Ilionekana mwanzo kama jeraha la mchezaji huyo halitakua kua kubwa lakini madaktari wa timu hiyo wamegundua hawakulichukulia kwa ukubwa jeraha hilo lakini kumeibuka hofu huenda Neymar akakosekana kwenye michuano hiyo.
Timu ya taifa ya Brazil mwaka huu imeandamwa na majeraha kwa kiwango kikubwa kwani mpaka sasa takribani wachezaki wanne wamepata majeraha huku wawili wawili ni rasmi hawatakuepo kwenye michezo iliyobakia ambao ni Alex Telles pamoja na Gabariel Jesus.

